Saturday, August 08, 2009


Enzi hizo ukiona 'Mtemba' kama huu unaondoka Bandari ya Salama basi unajua kabisa kuwa panga pangua humo ndani hamkosi vijana wetu wawili watatu wamedandia kwenda kutafuta maisha Ulaya! Siku hizi sina hakika hata kama wanajua neno 'Mtemba'!
Posted by Picasa

Wabongo! Labda tujaribu kuandika kinyume ndio watu wataelewa! Ukitaka watu wasitupe takataka mahali basi wewe andika 'Ni RUHUSA KUTUPA TAKATAKA HAPA'!
Posted by Picasa

Thursday, August 06, 2009


Kwa hadhi yake na eneo iliyopo, tunategemea wazee wetu wa Mpira waingie mikataba na wazee wa ujenzi kama NSSF na NPF (Nasikia ni mashirika ya Akiba za Wafanyakazi!) ili watujengee 'Kitu' chenye hadhi zaidi ya hiki!
Posted by Picasa

Tairi limechomoka. Mwisho wa safari. Marejesho ya Nauli!
Posted by Picasa

Uongo mbaya, Bongo siku hizi mambo sio mabaya sana kwenye suala la kujenga 'Vibanda'...!
Posted by Picasa
Posted by Picasa

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Moshi, Muuza Duka mmoja Mbunifu alichoka kuibiwa vitu vyake na kuamua kumnyoa Mbwa wake kwa staili ya Simba Shave! Taarifa ni kwamba hakuna Kibaka anayesogelea Duka hilo sasa Hivi! Habari/Picha kwa hisani ya Blog ya Brother Adam Lusekelo.
Posted by Picasa

Michael Jackson ...Alikuja...Akaona...Akatawala Ulimwengu wa Muziki...Ameondoka.
Posted by Picasa

Baada ya kutimuliwa Jangwani, ambapo pia yameisharudi tena, magari makubwa yamevamia mitaa yetu ya uswahilini na kufanya ndio Parking zao!
Posted by Picasa