Wednesday, February 27, 2008


'Stendi ya mabasi Ubungo' ya Bumbuli 'City'...!
Posted by Picasa

5 comments:

Anonymous said...

Hilo basi hapo kwa vyovyote ni Najims tena lile la kwanza maana nasikia lile jipya limeua dereva wake, hapo ndio mjini kwetu wakati wa pasaka na sikukuu bila kupita maeneo hayo sikukuu haijanoga halafu usubiri mabasi yakiingia jioni upate udaku wa mjini, nani kaja kwenye sikukuu nani hajaja

Anonymous said...

broo tunaomba ukienda kwenye krismas mwaka huu usikose kutuletea picha za huko kijijini tunakumbuka nyumbani lakini tuko mbali sana nauli tunatafuta mwaka, naomba picha za wazee wafuatao kama wako hai, Mzee Tadeo mwalimu na mpiga tarumbeta na kaka yake mzee kighobo yule mchungaji aliyekuwa anaongoza ibada bila kuchungulia kitabu mwanzo hadi mwisho,alikufa mwanafunzi pale maduda basi babu akaja kumzika, kila mwanafunzi hakuwa attention kwenye msiba ila kwa babu alivyokuwa akitema injili bila kusoma popote, nisalimie kama yupo, anakaa na wajukuu zake pale msasa,mpitie nijue habari zake. Mzee Dilli pale stand,mzee sefu aliyekuwa na hotel,mzee kinyata aliyeoa mtoto wa mzee sefu,Mch.Kusaga,Mzee abrahamu mpiga kinanda,mzee mshambaa mjanja alikuwa na duka zuri pale stand juu

Anonymous said...

Annony wa 17:06 nahisi kuwa utakuwa
umetoka nyumbani muda mreeefu sana na hujapata kurudi katika siku za karibuni. nasikitika sana kukuambia kuwa hao wote uliotaja wameisha tangulia mbele za haki kati ya miaka mitano hadi kumi iliyopita. Huyo mzee Mshambaa mjanja hata mtoto wake Salehe naye aliishafariki mwaka juzi. Huyo mzee Dili mtoto wake anayeitwa Bob naye aliishafariki.

Anonymous said...

Baaaaaaaaad news to me bro, sio kuwa nimeondoka siku nyingi hapo Bumbuli ila nilisoma tu pale enzi za Mwl.Mguhi wakati akifundisha msongolo na baada ya kupasi na kuondoka sijarudi tena Bumbuli na sina taarifa zozote,ila hili jina lako nilijua kwani siti nilisoma naye usagara nikajua ni ndugu yako

Anonymous said...

...Ok. Atafurahi sana kama akipata taarifa zako. Yupo bumbuli amestaafu. nitumie kwenye chesimpilipili@gmail.com.